Background Image
Previous Page  20 / 68 Next Page
Information
Show Menu
Previous Page 20 / 68 Next Page
Page Background

Ulevi unasababisha hatari za kudumu kwa binadamu. Utandawazi

umesababisha mabadiliko katika mienendo ya kimaisha, na

umewezesha upatikanaji wa madawa ya kulevya na teknolojia mpya

za kulevya kwa urahisi zaidi. Kwa kuwa zinasambazwa kwa haraka

sana, harakati za kupigana dhidi ya ulevi zimekubwa na vikwazo

tele. Dakt. Mehmet Dinç ambaye ni Rais wa muda wa Green Crescent

amesisitiza kwamba kwa sababu hiyo, jitihada zaidi zilenge hatua za

kutoa kinga, na aliongeza kwamba “Sisi kama Green Crescent, hadhira

lengwa yetu ni binadamu wote. Tunajitahidi kuhakikisha kwamba

walioelemewa na ulevi wanaweza kujikokota kutoka shida hiyo,

wakati pia tukitoa kinga kwa wale ambao hawajalewa ili wasilewe.

Shabaha yetu ni kuona afya njema na furaha kwa binadamu wote.

Utafiti umeonyesha kwamba licha

ya jitihada kubwa za kupambana

na ulevi ulimwenguni kote, tatizo

hili linazidi kuongezeka. Kwa maoni

yako, jitihada za kupigana na ulevi

zimefaulu kwa kiasi gani, na tafiti

ambazo zimefanywa hadi sasa

zinatosha?

Kwa kuwa ulevi ni jambo linaloathiriwa

na

mambo

kadha,

limekuwa

tatizo kubwa sana ambalo linazidi

kuongezeka duniani. Ongezeko la tatizo

hili kila kuchao haimanishi kwamba

nchi, mashirika, asasi za kiafya na vyuo

vikuu havijishughulishi na utafiti wa

kutosha kuhusu tatizo hili. Kinyume ni

kwamba asasi hizi zimefanya shughuli

baada ya shughuli na kuandaa miradi

kadha wa kadha kwa madhumini ya

kupigana na ulevi. Lakini, kiwango

ambacho tumefikia na habari ambazo

tumekusanya hadi sasa zinaonyesha

kwamba tafiti zilizokwisha fanywa

hazitoshi kulikabili vyema tatizo la

ulevi. Katika ulimwengu wa sasa, ulevi

ni tatizo lenye nyuso mbalimbali na

linalosambaakwakasi tele; kasi ambayo

inakuwa vigumu sana kwa tafiti zilizopo

kustahimili, na mabadiliko baina ya

tafiti hutokea kwa haraka sana.

Una maoni gani kuhusu sababu za

ongezeko la ulevi katika ulimwengu

wa lleo?

Kila

taaluma

imekumbwa

na

mabadiliko ya haraka sana duniani

kote. Kuanzishwa kwa utandawazi

katika maisha yetu kumesababisha

misimamo

ya

kifikra

ya

watu

kudhoofika polepole kwa kufungamana

na mabadiliko ya mienendo ya maisha

kutoka juu hadi chini, na kusababisha

kuvunjika kwa mahusiano baina ya

watu, na mwanzo wa mitafaruko ya

kijamii na matatizo ya kiuchumi. Sasa

ningependa kurejelea mfano mwepesi

sana. Msimamo wa kifikra wa mtu

unapodhoofika polepole, nia yake ya

kushikilia jambo fulani huongezeka.

Makampuni yauzayo vifaa vya kulevya

hulenga haja hii ya mtu, na kuleta vifaa

vya kulevya kwa jamii hizo na kwa watu

kama suluhisho lepesi na la haraka.

Picha zilipigwa na: Halil Altınta

DAKT. MEHMET DİNÇ,

RAIS WA MUDA WA GREEN CRESCENT:

“TUNALENGA AFYA

NJEMA NA FURAHA

KWA BINADAMU

WOTEY”

Alisoma shahada yake ya elimu kwa Idara

ya Masomo ya Ushauri na kutuliza Akili

ya Chuo Kikuu cha Marmara. Alisoma

shahada ya uzamili katika Elimu kutoka

Chuo Kikuu cha RMIT na shahada nyingine

ya uzamili katika masomo ya Saikolojia ya

Kimatibabu kutoka Chuo Kikuu cha Okan,

kisha alipata shahada ya uzamivu kutoka

Chuo Kikuu cha Marmara. Aliteuliwa

kuwa Rais wa Chama cha Washauri wa

Kisaikolojia na Chuo cha Australia nchini

Uturuki. Hivi sasa yeye ni mhadhiri katika

idara ya Saikolojia ya Chuo Kikuu cha

Hasan Kalyoncu. Sasa hivi yeye ni Rais wa

muda wa Green Crescent; pia Mjumbe wa

Bodi ya Chama cha Utamaduni , Jamii

na Familia; na pia wakala wa Uturuki

kwenye Kituo cha Dulwich cha Matibabu

ya Kinathari; na pia wakala wa Uturuki kwa

Chama cha Waliowahi kusoma Cho Kikuu

cha RMIT; na mjumbe wa Bodi ya Ushauri

ya Jarida la Matibabu ya Kisaikolojia na

Tabia za Kiakili na Utafiti.

Ameandika vitabu vitatu vyenye vichwa

İnternet Bağımlılığı, Gençliğe Kitabe na

Psikolojiye Giriş, na pia amekuwa na miradi

ya uandishi wa pamoja na Profesa Dr.

Kemal Sayar. Pia ameandika sura kwenye

vitabu 8.

DAKT. MEHMET DİNÇ NI NANI?

18