Background Image
Previous Page  26 / 68 Next Page
Information
Show Menu
Previous Page 26 / 68 Next Page
Page Background

Gilberto Gerra, MD, Mkuu wa Idara ya Kuzuia Madawa ya kulevya na Afya

chini ya Idara ya Utendaji ya UNODC, ambaye ni mwanasayansi mashuhuri

katika mapambano dhidi ya madawa ya kulevya anasema kwamba;

“UNODC inaangazia kwamba Green Crescent itafanya kazi kubwa ya

kiuongozi imara katika kiwango cha kimataifa katika miaka ijayo.”

Je, Unaweza kutwambia msimamo

wa dunia kuhusu utumiaji wa

madawa ya Kulevya?

Uraibu wa madawa ya kulevya

hutambuliwa kama shida tata ya

kiaafya iliyo na njia maalum ugonjwa

unavyokua

yaani

pathogenesis

inayoweza kuepukwa na kutibibika.

Mifumo ya zamani ambayo kwayo

utumiaji wa madawa ya kulevya

uliangaliwa kama uhalifu, upungufu

wa maadili, kama zoezi la burudani au

hali ya jamii, vimepitwa na wakati.

Kwa Kufuatia Kikao Maalum cha

Mkutano Mkuu wa Umoja wa

Mataifa kuhusu Tatizo la Madawa ya

Kulevya Duniani mnamo 2016, nchi

wanachama zilitambua umuhimu wa

kufuata mtazamo wa kiafya kuhusu

utumiaji wa madawa ya kulevya na

shida za utumiaji wa madawa ya

kulevya, wakajitolea “kukuza afya,

ustawi na afya njema ya watu wote,

familia na jamii kwa ujumla, na

kuwezesha maisha yenye afya njema

kupitia mipango madhubuti, kamili,

ya kisayansi ya kupunguza mahitaji

ya madawa ya kulevya katika ngazi

zote ... “(Hati ya Matokeo ya UNGASS,

uk. 4). Hii ni ishara ya daraja ambalo

limejengwa kati ya sayansi, sera

ya madawa ya kulevya na utendaji,

vinavyosababisha huduma kamili kwa

wagonjwa na wateja kote duniani

Je! Ni nini kinachofanywa kulinda

afya ya umma ya ulimwengu, na ni

nini kimepangwa kwa siku zijazo?

Katika kipindi cha miaka 12 iliyopita,

Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya

madawa ya kulevya na Jinai (UNODC)

imefanya kazi katika nchi zaidi ya

50 ili kuelekeza zaidi uongezekaji wa

bingwa na wataalamu katika uwanja

wa tiba ya madawa ya kulevya na

imejaribu mipango ya kuzuia utumiaji

wa madawa ya kulevya kwa kuegemea

ushahidi mkali kwa shule na familia.

Hili limefanywa kupitia utengenezaji

wa hati za kuonyesha mazoezi,

kama vile Viwango vya Kimataifa

vya Kuzuia Matumizi ya madawa ya

kulevya vya Kimataifa vya Tiba ya

Matatizo ya Matumizi ya madawa ya

kulevya zilizofanywa kwa kushirikiana

na Shirika la Afya Duniani. Kwa

kuongezea, UNODC imeongeza uwezo

wa watunga sera na watendaji kupitia

mafunzo mengi na mipango ya

uongozi.

Pamoja na mabadiliko ya mtazamo

wa kiafya wa dunia, nchi Wanachama

zimeanza kuhama kutoka mtazamo

wa kuweka vikwazo na kuadhibu na

kuanza kutumia mtazamo wa utunzaji

wa afya na kukubaliwa kwa waraibu na

jamii, na UNODC imewezesha mbinu

inayoangazia mwendelezo wa utunzaji

wenye mwelekeo wa kuponnya, kutoa

mahitaji maalum ya mtu aliyeathiriwa

katika nyakati tofauti za ugonjwa.

Nchi wanachama zinapaswa kuhama

kutoka kwa hatua zilizofanywa kwa

kutengwa na kuchukua mitazamo

unaounganisha njia za kisaikolojia

ya jamii na kifamasia, ikijumuisha

Mahojiano na: Fatıma Aydın

GILBERTO GERRA, MD:

“GREEN CRESCENT

YAENDELEA KUWA

KIONGOZI MKUBWA

WA DUNIA”

Gilberto Gerra, MD, alizaliwa huko

Parma, nchini Italia. Alimaliza masomo

yake ya chuo kikuu katika Shule ya

Tiba ya Chuo Kikuu cha Parma. Hivi

sasa anafanya kazi kama mtaalamu

wa magonjwa ya watu wazima na

daktari wa mfumo wa tezi yaani

endocrinologist. Wakati wa kazi yake

ya kitaalam amefundisha katika vyuo

vikuu vingi nchini Italia katika uwanja

wa nyurodokrinolojia na maduka

yanayouza dawa bila kufanya vipimo

vya kimaabara . Alifanya kazi katika

Kituo cha Matibabu ya Madawa ya

Kulevya huko Parma kati ya mwaka

1982 na 2003, akafanya kazi kama

Mkurugenzi wa taasisi hiyo kutoka

1995 hadi 2003, na katika kipindi

hicho hicho alifanya kazi pia kama

Mkurugenzi wa Kituo cha Utafiti wa

Uraibu wa madawa ya kulevya huko

Parma.

Kisha akaendelea kuwa Mkurugenzi

wa Uchunguzi wa Kitaifa wa madawa

ya kulevya wa katika Ofisi ya Waziri

Mkuu, Roma, Italia, na alikuwa

Mwanachama wa Bodi ya Kimataifa

ya kudhibiti madawa ya kulevya ya

Nakotiki (INCB) kwenye Umoja wa

Mataifa, huko Vienna. Tangu 2007,

amefanya kazi kamaMkuu wa Tawi la

Kuzuia madawa ya kulevya na Afya,

Idara ya Operesheni, Ofisi ya Umoja

wa Mataifa ya madawa ya Kulevya na

uhalifu huko Vienna.

KUHUSU GILBERTO GERRA, MD

24