Background Image
Previous Page  35 / 68 Next Page
Information
Show Menu
Previous Page 35 / 68 Next Page
Page Background

“GREEN CRESCENT LIMEKUWA JAMBO

KUU KWA UOKOAJI WA MAISHA YANGU ”

Sasa M.T. na familia yake wanayo maisha

mazuri na ya furahawakati ujao; shukrani

kwa Kituo cha Mafunzo na ushauri cha

Green Crescent ambacho kilikuwa hatua

ya kwamba katika harakati zake za

kujiondoa kutoka minyororo na athari

za ulevi wa pombe aliouingia alipokuwa

mdogo sana. Kama waathiriwa wengi

wa ulevi, M.T mwenye umri wa miaka 58,

hakuuona ulevi wa pombe kama shida

maishani mwake. Lakini, ni mke wake

na watoto ambao walisumbuliwa na M.T.

kunywa pombe na harakati za mwanzoni

za kumwokoa M.T. kutokana na pombe

zilifanywa nao yaani mke na watoto

wake. M.T. alikunywa pombe kuanzia

miaka yake ya ujana hadi miaka 58, lakini

aliweza kubadilisha na kuiacha tabia ya

ulevi kwa usaidizi wa Kituo cha Mafunzo

ua ushauri cha Green Crescent.

Msaada unaosababisha uokoaji

Familia ya M.T. iliyompenda sana,

lakini ikasumbuliwa sana kuishi na

mtawaliwa/mraibu wa pombe, ilianza

safari ya kumwokoa M.T, iliyoanza na

maombi yake kwa Kituo cha Mafunzo na

Ushauri cha Green Crescent. Kwa miaka

minne, wanasaikolojia wa Kituo cha

Mafunzo na Ushauri cha Green Crescent

wafanya mahojiano na mke wake

M.T. na watoto wake watatu. Baada ya

kutambua kwamba familia yake ilikuwa

imebadilika, M.T. aliuliza ni wapi na

kutoka kwa nani familia yake walikuwa

wakipokea msaada, jambo lililompelekea

kutembelea Kituo cha Mafunzo na

Ushauri cha Green Crescent kuona

kinachoendelea. M.T. alivutiwa sana na

upendo na utunzaji aliopewa na familia

yake na wanasaikolojia wa Kituo cha

Mafunzo na Ushauri ya Kijani cha Green

Crescent. Katika mahojiano yake ya

kwanza, M.T. alisema kwamba hakuhitaji

matibabu wala hakutaka kulazwa

hospitalini. Anaendelea kuzungumza juu

ya hatua iliyofuata katika mchakato huu:

“Nilijifunza kuwa inawezekana kupokea

ushauri tu bila kupewa matibabu. Hii

ilikuwa nafasi kubwa maishani mwangu.

Nilidhani, angalau hawatajaribu kunitibu

kwa nguvu, kwa hivyo nilianza kupata

ushauri nasaha. Sikumoja, bila kuijulisha

familia yangu, nilichukua miadi kutoka

kwa Kituo cha Mafunzo na Ushauri Green

Crescent ili kuanza kupata matibabu.

Nilitaka kubadilisha maisha yangu na

hali yangu. Nilikuwa na familia iliyokuwa

ikinipigania, pamoja na wanasaikolojia

wa Kituo cha Mafunzo na Ushauri wa

Kijani cha Green Cresent”

Matibabu ambayo yalibadilisha

mtazamo wangu wa maisha.

Wanasaikolojia wa Kituo cha mafunzo

na ushairi cha Green Cresent walijibu

maswali kuhusu uraibu wa pombe

na matibabu, na baada ya kuiona

familia yake ikiendelea na mahojiano

bila kuchoka, M.T, akapata mwamko

uliompelekea kikiri kwamba alikuwa na

shida kubwa sana na pombe. M.T alianza

mchakato wa kutibiwa katika Kituo cha

Mafunzo na Ushauri cha Green Crescent

kinachotoa huduma za bure za saikolojia

kwa watu wanaotawaliwa na uraibu wa

madawa na pombe pamoja na familia

zao. Bado anapata matibabu lakini kwa

sasa anaona mafanikio makubwa na

kutazamia maisha bora wakati uajo.

M.T. ni mwathirika wa pombe ambaye maisha yake yalikuwa yameathiriwa vibaya, lakini baada ya hapo aliweza

kubadilisha maisha yake wakati tu alikuwa karibu kupoteza familia yake na rasilmali yake yote. Sasa M.T. na

familia yake wanaona maisha mazuri siku zijazo; shukrani kwa maombi yake aliyotuma kwa Kituo cha Mafunzo

na Ushauri cha Green Crescent, ambayo (maombi) yalikuwa hatua yake ya kwanza kujiondoa kutokana na athari

za pombe. Kituo cha Mafunzo na Ushauri cha Green Crescent kimekuwa “jambo muhimu kwake”, anasema M.T.

33