Background Image
Previous Page  38 / 68 Next Page
Information
Show Menu
Previous Page 38 / 68 Next Page
Page Background

Kila mwaka, watu milioni saba duniani hufariki kutokana na magonjwa

yanayojihusisha na uvutaji sigara, jambo ambalo linasababisha

uzinduzi mkubwa wa mapambano dhidi ya mazao ya tumbaku.

Prof. Dkt. Toker Ergüder, Mkurugenzi wa Mpango wa Magonjwa

yasiyoambukiza katika Afisi za Shirika la Afya Duniani nchini Uturuki

aliorodhesha umuhimu wa mapambano dhidi ya Tasnia ya Tumbaku

akisema kuwa “Tumbaku ni tathnia kubwa na yenye faida kubwa

duniani.”

Unaweza kutoa mhutasari wa

msimamo wa Dunia nzima kuhusu

Uraibu wa Tumbaku?

Utumiaji wa tumbaku unaongoza

katika

usababishaji

wa

vifo

vinavyoweza kuzuiliwa nchini Uturuki

na Dunia nzima kwa ujumla; na

sekta ya tumbaku ndiyo inayoongoza

katika usambazaji wa magonjwa ya

mlipuko na hatari yanayohusiana na

tumbaku. Sasa, kuna mbinu kadhaa

zinazofaa na tafiti kuhusu uzuiaji wa

ulevi wa tumbaku, ingawa ni muhimu

kufahamu kwamba mapambano dhidi

ya utumiaji tumbaku sio mapambano

dhidi ya wavutaji sigara. Kwa kweli,

tunajaribu kuwasaidia wavutaji sigara

kuacha uvutaji na kuwasaidia kuishi

maisha yasiyoathiriwa na uraibu wa

kuvuta sigara. Baada ya kusema hayo,

mapambano yetu makuu yako dhidi

ya kampuni za sigara na tasnia ya

tumbaku. Tunaweza kusema kwamba,

tasnia ya tumbaku ndiyo tasnia kubwa

yenye faida kubwa duniani na takwimu

zilizopo zinthibitisha dai hili. Katika

mwaka wa 2017, mauzo ya rejereja ya

sigara yalifika takribani bilioni 700 za

Dola ya Marekani na hili linamaanisha

kwamba sigara trilioni 5.4 ziliuzwa

mwaka huo. Azma kuu ya tasnia ya

tumbaku ni kufungua mlango wa

uraibu wa uvutaji sigara kwa kuingiza

watoto na vijana yaani mvuto mmoja

wa tumbaku kabla hawajabarehe.

Tasnia ya tumbaku hufanikiwa katika

kampeni na mikakati yake sambamba

na malengo yake hatari. Takribani

watu milioni 7 duniani hufariki kila

mwaka kwa sababu ya magonjwa

yanayohusiana na uvutaji sigara,

huku watu milioni 1 wakifariki kwa

kuukaribia moshi wa sigara. Matumizi

ya tumbaku ni jambo hatarishi

katika vitu 6 vinavyojulikana sana

kusababisha vifo duniani kati ya 8.

Mogonjwa yamoyo, yanayosababishwa

na mishipa ya moyo kuwa nyembamba

hali inayosababisha damu kidogo na

oksijeni kufikia misuli ya moyo na

hivyo kusababisha shinikizo la damu,

magonjwa yanayohusiana na uharibifu

wa neva zinazosafirisha oksijeni

kwenye ubongo na kusababisha

kutokuwepo kwa oksijeni ya kutosha

kwenye ubongo, maambukizo ya njia

ya chini ya kupumua, magonjwa sugu

ya mapafu, kifua kikuu na saratani

zote za mapafu husababisha vifo

vinavyojihusisha na uvutaji sigara.

Saratani ya mdomo na ya koromeo,

saratani ya umio, saratani ya tumbo

na saratani ya mapafu huchangia sana

katika vifo vinavyohusiana na uvutaji

sigara.

Idadi kubwa ya wavutaji sigara

katika nchi zilizoendelea na nchi

zinazoendelea

huongeza

vifo

vinavyohusiana na uvutaji sigara

katika nchi hizi. Kwa kweli, tukiangalia

kwa mtazamo wa dunia, tunaona

kwamba ueneaji wa uvutaji sigara

unapungua, aidha hili lisiwapotoshe

wale wanaoshiriki katika mapambano

dhidi ya uraibu huu. Ingawa viwango

vya uvutaji sigara vimepungua haswa

Mahojiano na: Fatıma Aydın

PROF.DKT.

TOKER ERGÜDER:

“TUNAHITAJI

KUPAMBANA DHIDI YA

TASNIA YA TUMBAKU”

Prof. Dkt. Toker Ergüder ni Daktari wa

Matibabu na mtaalamu wa Afya ya Jamii

ambaye anafanya kazi kama Mkurugenzi

wa Mpango wa magonjwa yasioambukiza

katika Afisi za Kimkoa za Shirika za Afya

Duniani (WHO) nchini Uturuki. Pia, Prof.

Dkt. Toker Ergüder ni mhadhiri katika

Idara ya Afya ya Jamii, Kitivo cha Tiba

Gülhane, Chuo Kikuu cha Sayansi ya Tiba.

Yeye anatoa usaidizi wa kiufundi kwa

Wizara ya Afya, kwa mashirika yasiyo

ya Kiserikali na kwa mashirika mengine

yanayohusiana na udhibiti, na usimamizi

wa magonjwa yasiyoambukiza nchini

Uturuki na mapambano dhidi ya utumiaji

wa tumbaku. Yeye ni mwanachama wa

Kamati ya Kisayansi ya Green Crescent.

Kabla yakuchukua majukumu kadhaa

katika Shirika la Afya Duniani, alifanya

kazi katika Wizara ya Afya kati ya 2002 na

2007 na kuanzisha Idara ya kupambana na

tumbaku.

Mnamo 2003,alianza kufanya juu chini

ili nchi ya Uturuki itie sahihi Mkataba wa

Mfumo wa kudhibi tumbaku na katika

uanzishaji wa Udhibiti wa Taifa wa

Tumbaku. Mnamo 2007, Gülhane alitoa

mchango mkubwa katika kutengeza upya

sheria Na. 4207 iliyoifanya nchi ya Uturuki

kuwa eneo “lisilo na Moshi wa sigara” kwa

maagizo ya Rais Recep Tayyip Erdoğan

PROF. DKT. TOKER ERGÜDER NI NANI?

36