Background Image
Previous Page  43 / 68 Next Page
Information
Show Menu
Previous Page 43 / 68 Next Page
Page Background

Kupitia mpango wake

wa Msaada wa kifedha,

Green Crescent inasaidia

mashirika ya Kitaifa ya

Green Crescent katika

juhudi zao za kuimarisha

uwezo, ili kufanya kazi za

kisayansi, na kuchukua

jukumu muhimu katika

sera za kupambana na

ulevi katika maeneo yao.

MASHIRIKA YA KITAIFA YA GREEN

CRESCENT YASHAMIRI KUPITIA MPANGO

WA MSAADA WA FEDHA WA KIMATAIFA

G

reen

Crescent

inaendelea

kutoa msaada kwa mashirika

ya kitaifa ya Green Crescent katika

mapambano yao dhidi ya uraibu wa

madawa ya kulevya katika pembe

zote nne za dunia kupitia Mpango

wake wa Kimataifa wa Usaidizi wa

Kifedha. Mpango wa Msaada wa

kifedha wa Kimataifa wa Green

Crescent unakusudia kuhakikisha

uimarikaji wa kitaifa wa mashirika

ya Kitaifa ya Green Crescent, huku

pia ukiongeza uwezo wao, na

kushawishi sera za kupambana

na uraibu wa madawa ya kulevya

kujenga miundombinu ya utetezi.

Kuhimiza mashirika ya kitaifa ya

Green Crescent kutekeleza utetezi,

utafiti wa kisayansi na majukumu

ya kuzuia uraibu wa madawa ya

kulevya katika nchi zao, Mipango

ya Msaada wa kifedha ya Kimataifa

imekusudiwa pia kusaidiamashirika

ya Kitaifa ya Green Crescent katika

kupata

miundombinu

muhimu

ya kiufundi ambayo itawaruhusu

kufanya kazi kwa ufanisi zaidi

Mpango unaotekelezwa katika

nchi 26

Huku likijitahidi kuendelezaMpango

wake wa Kimataifa wa Usaidizi wa

Fedha wa mwaka wa 2019, Mpango

wa Msaada wa Fedha wa Kimataifa

wa Green Crescent wa mwaka 2017

sasa umetekelezwa katika nchi 26,

zikiwemo; Afghanistan, Albania,

Australia,

Azabajani,

Bosnia-

Herzegovina, Bulgaria, Jamhuri

ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC),

Kupro, Georgia, Indonesia, Kenya,

Kosovo,

Kyrgyzstan,

Lebanon,

Makedonia, Malaysia, Montenegro,

Moroko, Niger, Nigeria, Palestina,

Serbia, Somalia, Sudan, Syria na

Uganda. Mpango wa Msaada wa

Fedha wa Kimataifa wa mwaka wa

2019 hivi sasa inaandaliwa.

Maeneo ya kazi

Shughuli

zifuatazo

zinafanywa

katika Mpango wa Msaada wa

Fedha wa Kimataifa: “Kurekebisha

maudhui ya vifaa vya kuzuia

uraibu wa madawa ya kulevya

yalivyoundwa na Green Crescent

katika nyanja za uzuiaji na utetezi

kuhusu mapambano dhidi ya uraibu

wa madawa ya kulevya kwa hali ya

kiuchumi jamii ya nchi inayohusika,

na kufanya utafiti wa nyanjani;

kuunda mitandao ya ushirikiano

wa kitaifa na wa kimataifa; na

kuboresha mwingiliano wa kikanda

kati ya mashirika yote ya Green

Crescent,

kuyaruhusu

kupata

rasilimali muhimu za kiufundi

ambazo

zitawaruhusu

kufanya

kazi vizuri; kupitia maandishi ili

kujua hatari za uraibu wa madawa

ya kulevya katika viwango vya

kikanda na kitaifa; na kutoa ripoti

ya matokeo ya utafiti baada ya tafiti

za makundi kufanywa. “

Sampuli ya miradi

Kuandaa mashindano ya ‘Kizazi

cha Afya bora, Maisha bora ya

kiafya ya siku zijazo” katika ngazi

ya jimbo, kimkoa au kitaifa;

Kurekebisha maudhui ya TBM

yaani; mpango wa Mafunzo

ya kuzuia uraibu wa madawa

ya kulevya nchini Uturuki) na

kutekeleza mpango(wa walimu wa

mafunzo/walimu/walimu wa rika);

Urekebishaji na utekelezaji wa

Mradi wa Green Crescent ‘Chama

Changu’;

Kuandaa mashindano ya video

fupi na kampeni ya mawasiliano;

Kuwafahamisha vijana, wazazi

na wadau wengine kuhusu hatari

za uraibu wa madawa ya kulevya

na kuandaa semina na warsha ili

kuhamasisha jamii;

Kuanzisha klabu/vyama vya Green

Crescent katika vyuo vikuu;

Kukuza shirika la Green Crescent

la kitaifa; kuihamasisha umma

kupitiamatangazonakuwahusisha

watu kama wafanyakazi wa

kujitolea, wanachama, n.k.

41