Background Image
Previous Page  46 / 68 Next Page
Information
Show Menu
Previous Page 46 / 68 Next Page
Page Background

Prof. Mshiriki, Dakt. Perihan Torun ambaye ni kiongozi wa utafiti wa

sera za Uturuki kuhusu Udhibiti wa Pombe wa Kimataifa, alisema:

“Madai kwamba kuna manufaa yanayotokana na kutumia kiasi fulani

cha pombe hayana mashiko, kwani uchunguzi uliofanyika hivi juzi

umekadiria kwamba mzigo wa dunia wa maradhi yanayotokana na

utumiaji pombe yanaongezeka sambamba na ongezeko la kiasi cha

pombe kinachotumika.”

Ungefafanuaje kiasi cha pombe

kinachotumika duniani hivi sasa?

Shirika la afya la Dunia (WHO)

limeripoti kwamba takribani nusu ya

watu duniani wenye umri wa miaka

15 na zaidi hawajawahi kuonja pombe.

Pombe inatumiwa na zaidi na nusu ya

watu katika maeneo ya WHO matatu

kati ya sita, yaani maeneo ya Bara

ya Amerika, Ulaya na Mashariki ya

bara ya Pasifiki ambako utumiaji

pombe huanza kabla ya mtu kutimia

umri wa miaka 15. Katika miaka

michache iliyopita, kiasi cha pombe

kinachotumiwa kinasemekana kuwa

kinaongezeka katika maeneo ya WHO

ya kusini-magharibi ya Pasifiki na

Kusini ya Asia, na kupunguka katika

eneo la Ulaya.

Nchi zenye idadi ya chini ya

watumiaji pombe, zile zisizo na

sera kali za kudhibiti pombe na/

au zisizotekeleza sera za kudhibiti

pombe zina nafasi kubwa ya kuvuta

kampuni zinazotengeneza na kuuza

pombe kama masoko yatakayoleta

faida. Imeripotiwa kwamba shughuli

za kibiashara za sekta ya pombe

zinaongezeka katika nchi za Kiafrika,

na kwa sababu hiyo, madhara

yanayotokana na utumiaji pombe

yanatarajiwa kuongezeka. Isitoshe,

kwa kuwa utumiaji pombe unaripotiwa

kuongezeka pale kipato cha watu

kikiongezeka, nchi ambazo zina

uchumi unazidi kukua zina uwezekano

mkubwa wa kuathirika sana.

Ushahidi wa madhara ya utumiaji

pombe umekuwa ukizidi kuibuka

ndani ya mwongo uliopita kutoka

tafiti zilizotumia taratibu bora za

utafiti. Madai kwamba kuna faida

fulani kutokana na kutumia pombe

zimepitwa na wakati, kwani tafiti

za hivi majuzi zimekadiria kwamba

maradhi yanayotokana na utumiaji

pombe duniani yanaongezeka kadri

utumiaji pombe unavyoongezeka. Sera

za kitaifa zinafaa kuzingatia ushahidi

huu uliopatikana kutokana na utafiti.

Ni hatua gani zinazochukuliwa kote

duniani ili kutunza afya ya jamii,

na kuna mipango gani ya siku za

mbele?

Ili kulinda watu dhidi ya madhara ya

pombe, ni muhimu kukusanya data

kuhusu kiasi cha utumiaji pombe

kwa watu binafsi, na data hizi zinafaa

kuzingatiwa wakati wa kutunga sera za

kudhibiti pombe.

Shabaha namba 3.5.2 ya Malengo ya

Maendeleo Endelevu (SDGs), ambayo

inalenga kiasi cha utumiaji pombe

cha kila taifa, inahitaji ufuatiliaji

wa utumiaji pombe. Shida inaibuka

katika shabaha hii kwenye nchi zenye

makundi makubwa ya watu wengi

wasiokunywa pombe na ukosefu

wa data kuhusu kiasi cha utumiaji

pombe cha watu binafsi. Katika hali

hii, wakati wa kuhesabu kiasi cha

wastani cha utumiaji pombe, hesabu

inayozingatia utumiaji wa jumla wa

watu nchini huzingatiwa. Hali hii

huwa haitoi picha halisi ya kundi

kubwa la wasiokunywa pombe, hasa

wanawake, data zinazopatikana huwa

zinapotosha. Hii ni sababu mojawapo

inayoifanya pombe kutofikiriwa kuwa

chanzo cha hatari katika nchi zenye

kundi kubwa la wasiokunywa pombe.

Sababu nyingine ni kuhusisha utumiaji

pombe na misingi ya kidini na kisiasa,

na hivyo kutoa taarifa nyeti kuhusu

utumiaji pombe wa watu binafsi.

Katika jamii ambazo kunywa pombe

ni marufuku kwa wengi, kwa mfano

nchini Uturuki, ukubalifu wa sera za

kuhakikisha watu hawatumii pombe

lazima zijadiliwe kwani “wachache

wasiokunywa watachangia ongezeko

la utumiaji wa kiwastani”. Basi, utafiti

waweza kulenga kukusanya data

za wasiotumia pombe na sababu za

kutoitumia, pamoja na data za utumiaji

wa hatari.

Ingawa pombe si mada nyeti ya

utafiti kwa jumla, inaweza kuwa nyeti

kulingana na mazingira na utamaduni,

na kwa hiyo kuwahitaji watafiti

kuandaa tafiti zao kwa uangalifu. Pia,

tofauti na uvutaji sigara, utafiti wa

utumiaji pombe huhitaji utaratibu

Mahojiano na: Fatıma Aydın

PROFESA MSHIRIKI,

DAKT. TORUN:

“ULIMWENGU

UMEKUBALI MADHARA

YA POMBE”

Ni mtaalam wa afya ya jamii na pia

mwana academia ambaye anafanya

kazi nchini Uturuki. Ni mwanamke

ambaye amekuwa akiongoza Utafiti

wa Tathminiya Sera wa shirika la

Kimataifa la Kudhibiti Pombe wa

Uturuki tangu mwaka 2016.

PROFESA MSHIRIKI, DAKT. PERİHAN TORUN

44