Background Image
Previous Page  45 / 68 Next Page
Information
Show Menu
Previous Page 45 / 68 Next Page
Page Background

Ikumbukwe kwamba Mpango wa Uturuki wa

Kupambana na uraibu wa madawa umetajwa

kama “Utendaji Bora” katika ripoti ya EMCDDA, Işık

alisema kwamba Green Crescent inaheshimiwa

na kutambuliwa na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali

kama “kiongozi wa maoni” yanayoshughulikia

malengo sawa na yele ya Green Crescentduniani.

Shukrani kwa shughuli za mfano wa kuigwa:

“Pamoja na uzoefu wake wa karne, Green Crescent

anasema na kutenda kama “kiongozi wa maoni”

sio tu kwenye uwanja wa kitaifa, bali pia kimataifa.

Hali yake kama shirika linalohusika na mitandao

katika nchi 52 duniani kote ambayo inashiriki

uzoefu wake na Mashirika Mengine yasiyo ya

Kiserikalini kiashiria muhimu zaidi cha kazi yake

kama kiongozi wa maoni. Kazi zetu nzuri na miradi

ya mfano imesababisha sisi kuonekana kama

kiongozi wamaoni naMashirika Yasiyo ya Kiserikali

yanazofanya kazi kwa malengo sawa ulimwenguni.

Mkutano wa leo wa Istanbul Initiative ni kiashiria

cha msimamo wetu kwenye jukwaa la Dunia. “

“Azimio ni hatua muhimu sana”

Akizungumzia kuhusu azimio hilo, , ambalo

linaelezea mikakati ya kiutendaji itakayochukuliwa

katika nchi zote zinazohusika katika mapambano

dhidi ya uraibu wa madawa ya kulevya, Işık alisema

kwamba, “Mbali na sababu za kijamii na kisaikolojia,

kuwepo watendaji wengineyapaswa kukubaliwa

kama nguvu kazi. . katika ongezekolamadawa

ya kulevya. Tatizo liko mielekeo anuai Mashirika

yasiyo ya Kiserikali yanaporudi katika nchi zao,

yanahitaji kushughulikia suala hilo katika kiwango

kinachokubalika na kiwango cha Umoja wa

Mataifa na mashirika ya kimataifa ya kiafya kama

vile; Shirika la Afya Duniani (WHO). Wanapaswa

kuzingatia mapambano haya kama jukwaa pana

ambalo wanahitaji kushirikiana mawakala wa

serikali na jeshi la polisi nchini mwao.. Azimio

la kujituma la Istanbul linajumuisha kanuni na

mapendekezo kama haya.”

“Tofauti za dawa zinaongezeka barani Ulaya”

Akirejelea Ripoti ya madawa ya kulevya na uraibu

wa madawa ya Kituo cha Ufuatiliaji wa madawa ya

kulevya za Ulaya (EMCDDA), Işık alisema kwamba

aina za dawa za kulevya huko Ulaya zimeongezeka:

“Ripoti hiyo inadokeza kuongezeka kwa utumiaji

wa aina mbili au zaidi za dawa ya kulevya (yaani,

polydrug) miongoni mwa watumizi wa dawa za

kulevya. Kuenea kwa bangi, kama dawa ya kulevya

inayotumiwazaidibaraniUlaya,ikojuuyamaratano

kulikomadawamengine ya kulevya. Hadi mwishoni

wamwaka 2018, zaidi yamadawa 730 ya kisaikolojia

yameripotiwa duniani kote, 55 kati ya madawa hayo

yamegunduliwa kwa mara ya kwanza mnamo 2018

huko barani Ulaya. Kwa bahati mbaya, Uturuki ni

nchi inayounganisha Ulaya na Mashariki ya Kati,

na kwa hivyo ni njia kuu ya biashara haramu ya

madaya ya kulevya kuna aina nyingi kutoka upande

wa Mashariki hadi wa Magharibi. Kama Green

Crescent, sisi ndio wasidizi wakubwa zaidi wa vijana

wetu na familia zao, tukishiriki katika kuzuia uraibu

wamadawa ya kulevya na ukarabati wa waraibu, na

kutoa msaada kuwafanya warudi na waanze kuishi

na bidamu wengine au kujumuishwa tena kwenye

jamii. “

MKAKATI WA ISTANBUL

Mkutano wa kwanza, Istanbul, Tarehe 12-13 JunI 2019

TAMKO

1. Idadi kubwa zaidi ya watu duniani hawatumii

madawa ya kulevya na wanataka kuishi kwenye

mazingira yasiyo na hatari zinazotokana na

kulewamadawa. Kundi hili ambalo ndilo kubwa

zaidi duniani linaunga mkono shughuli za

kuzuia ulevi wa madawa pamoja na kuwezesha

vijana na watu wengine walio hatarini kukuza

mikondo ya maisha, desturi na mazingira yenye

afya ili kuhakikisha upatikanaji wa afya bora na

maendeleo kwa wote.

2. Sisi, ambao ni wawakilishi wa mashirikia

yasiyo ya kiserikali ya kimataifa na ya kieneo

tuliotia saini hapo chini,

3. Tunatambua kwamba utumiaji pombe,

sigara, madawa ya kulevya na vifaa vinginevyo

vinavyochanganya akili husababisha madhara

ya kiafya, kijamii na kiuchumi kwa watu binafsi,

familia zao, jumuiya zao na jamii zao kwa jumla

na hatimaye kuhatarisha maendeleo endelevu.

4. Tunatanguliza afya na maslahi ya binadamu

wote, na kwa hiyo, tumesanyika kwenye

mkutano wa kwanza wa Mkaatati wa Istanbul

kutoa uamuzi kuhusu mahitaji ya vitendo vya

dharura vya kusuluhisha tatizo la madawa ya

kulevya duniani, mkiwemo ulevi wa vifaa na

tabia zinazochanganya akili;

5. Tunasisitiza kwamba kupunguza kiwango

cha upatikanaji wa madawa ya kulevya na

kuhakikisha kiasi chake kinakuwa chini sana

ndiyo njia bora zaidi ya kutoa kinga. Kutoa

kinga dhidi ya madhara ndiyo njia iliyo nafuu

zaidi inayozingatia utu na iliyo endelevu katika

kupunguza madhara yatokanayo na utumiaji

wa madawa ya kulevya, kuokoa masiha,

kuimarisha jumuiya mbalimbali, kukuza afya

ya jamii, maendeleo endelevu ya binadamu na

kupunguza matatizo yanayohusiana na ulevi.

6. Tunatambua kwamba sera za kukumbana

na madawa ya kulevya lazima zitungwe kwa

kuzingatia haki za kibinadamu, jinsia na umri;

7. Tunasisitiza umuhimu wa kuweka mifumo

ya kimatibabu inayolenga kuinua afya ya

wagonjwa wa ulevi, masuluhisho yanayojali

kila hali ya mgonjwa, kuanzia masuluhisho ya

awali hadi kupunguza madhara, kukarabati na

kumwezesha mgonjwa kukubaliwa tena katika

jumuiya yake, kwa lengo la kuwasaidia watu

walioathiriwa vibaya na utumiaji madawa ya

kulevya ili waweze kuishi maisha yenye fanaka.

8. Tunatambua

kwamba

madhara

yatokanayona na utumiaji madawa ya kulevya

hayaathiri tu mtu binafsi lakini pia yanaathiri

vibaya wachumba wao, wazazi wao, ndugu zao

na watoto wao; na kwa hiyo huduma thabiti za

usaidizi kwa familia na kwa watu wa uhusuano

wa karibu na mlevi wa madawa ni wa muhimu

sana katika kuzuia madhara na kujenga

misingi imara ya familia zenye stahamala;

9. Tunasisitiza umuhimu wa ushirika wa

wanajamii wote katika kukabili matatizo ya

utumiaji madawa ya kulevya kama jukumu la

kila mtu linalohitaji kukabiliwa kwa pamoja

kwa kuegemea ushahidi wa utafifi ili kubadili

sera, itikadi na mifumo katika viwango vyote

kupitia ushirikishaji wanajamii;

10.Kwa sikitiko kubwa tunafahamu hatari

za biashara za pombe na sigara, na sasa

tunasikitika zaidi kuona uibukaji wa biashara

mpya inayokuza utumiaji madawa ya kulevya

kwa faida ya watu binafsi, na kusababisha

madhara ya ajabu hasa kwa makundi ya watu

dhaifu na jamii kwa jumla.

11. Tunasikitika sana kuona biashara hii mpya

imeweza kupotosha ukweli na kuelekeza sera

za umma na kushawishi serikali, mashirika

ya kimataifa na mashirika yasiyo ya kiserikali

mbalimbali kwa ajili ya kufaidika kiuchumi,

kinyume na maslahi ya wanajamii;

12.Tunapigia mbiu watu wote, hasa viongozi

wa familia, kisiasa, kitamaduni, kidini, kiraia,

kiafya, kielimu, vijana, michezo, na biashara, na

vyombo vya habari kushiriki kwenye harakati

za kugeuza itikadi za kijamii, kupunguza

upatikanaji wa madawa ya kulevya, na kujenga

jamii zenye afya bora;

13. Tunapigia mbiu serikali zote na jumuiya ya

kimataifa kushikilia mkabala unaosawazisha

pembe zote za kupunguza kiasi na idadi ya

watumiaji madawa, kupunguza kiwango cha

uingizaji madawa na mamlaka za kuhakikisha

utendekaji wa sheria, na kuwekeza kwenye

harakati za kuzuia, kutibu na huduma za afya,

ili kufaulu katika kupata utulivu na ulinzi wa

kimataifa, na afya njema kwa mataifa;

14. Tunapigia mbiu serikali zote kuwekeza

kwenye mazingira yanayokuza afya bora ili

kufaulu katika kupata afya inayotamanisha,

neemai na maendeleo kwa watu wote;

15.Tunatamka nia yetu ya kuzidi kushirikiana

duniani kote kuunga mkono mipango

inayoshirikisha wanajamii wenyewe kwenye

mchakato wa utungaji sera wa kimataifa na

kupaaza sauti za kundi lililo kubwa zaidi la

wanajamiii wasiotumia madawa duniani kote.

43