Background Image
Previous Page  44 / 68 Next Page
Information
Show Menu
Previous Page 44 / 68 Next Page
Page Background

AZIMIO LA KIMATAIFA LILOFANYWA NA

“MPANGO WA KUJITUMA WA ISTANBUL”

GREEN CRESCENT

K

atika hafla iliyoandaliwa na Green

Crescent, wawakilishi wa Mashirika 21

yasiyo ya Kiserikali kutoka nchi 15 tofauti

mkiwemoUswidi, Ghana, Italia naMarekani,

walikutana tarehe 12-13 mwezi wa Juni.

Kutokana na mkutano uliofanyika katika

makao makuu ya Green Crescent katika

kioski ya Basketmakers huko Istanbul,

mpangompya uliwekwa katikamapambano

dhidiyauraibunamadawayakulevya.Wakati

wa mkutano, mashirika yanayoongoza

katika uwanja wa upambanaji na uraibu wa

madawa walijadiliana na kutoa maoni na

mapendekezo. Ilisisitizwa kwamba, hatua

za haraka haraka za dunia nzima zinapaswa

kuchukuliwa kushughulikia uraibu wa

madawa kwa sababu ya afya na ustawi wa

binadamu wote.

Katika tamko la pamoja, Mashirika

yasiyo ya Kiserikali yalisema “Acheni

utumiaji wa dawa za kulevya”

Katika kikao cha kwanza cha mkutano

huo, utakaofanyika huko Istanbul kila

mwaka, viongozi wa maoni ya umma katika

mapambano dhidi ya uraibu wa madawa

duniani kotewaliundampangowakimataifa

na kuandaa “Azimio la Kujituma la Istanbul”.

Likiwa na vifungu 15, tamko hilo liliwataka

viongozi wote wa maoni kutoka kwa

makundi mbali mbali, yakiwemo michezo,

afya, vijana na biashara, kubadili hali ya

kijamii ili kuzuia matumizi ya dawa za

kulevya na kujenga jamii zenye afya njema.

Tamko hilo pia lilithibitisha umuhimu wa

mifumo ya utunzaji inayolenga kuwaokoa

waraibu na kutoa hatua kamili, kuanzia

uokoaji mapema hadi upunguzaji wa hatari

yauraibu, nakutokakwaukarabati hadimtu

kuwa pona akaanza kusishi na binadamu

wengine. Kwenye mkutano na waandishi

wa habari uliofanyiwa katika mkutano huo,

Ripoti ya madawa ya kulevya 2019 ya Kituo

cha Ufuatiliaji wa Dawa za Ulaya na vile vile

ilishughulikiwa.

Wawakilishi waMashirika 21 yasiyo ya

Kiserikali kutoka katika nchi 15

Hotuba ya ufunguzi wa hafla hiyo ilitolewa

na Wakili Osman Baturhan Dursun, Katibu

Mkuu wa Green Crescent, ikifuatiwa na

maoni kutoka kwa viongozi mashuhuri

kamaRaiswa IOGTKristinaSperkovakutoka

Uswidi; Mwanzilishi na Rais wa KKAWF

Cristina Von Sperling Afridi kutoka Pakistan;

na Boro Goic wa RUN kutoka Bosnia na

Herzegovina. Mbali na Green Crescent,

wawakilishi wa asasi zinazoongoza katika

mapambano dhidi ya ulevi, kama vile;

CADCA, CADFY, Drug Policy Futures, , EURAD,

FORUT, IOGT, KKAWF, RUN, San Patrignano,

SCAD, mfuko wa pesa kwa ajili ya kutoa

msaada wa Sunny Trust, VALD, VNGOC na

WFADwalihudhuriaMkutanowa Kwanzawa

kujituma wa Istanbul.

Green Crescent: wanaongoza katika

mapambano dhidi ya uraibu wa madawa

duniani”

Kufuatia mkutano huo, Meneja Mkuu wa

GreenCrescent Sultan Işık alifanyamkutano

na waandishi wa habari pamoja na Kristina

Sperkova, Cristina Von Sperling Afridi na

Boro Goic na kujadiliana kuhusu tamko hilo

lililoandaliwa na makubaliano ya kawaida,

na kutoa habari zaidi juu ya Mpango wa

Istanbul.

Akisisitiza

kwamba

Green

Crescent

imekuwa ikifanya kazi na majukumu

muhimu tangu miaka ya 2000, Işık alisema

kwamba: Kupitia vituo vyetu vya Mafunzo

na Ushauri vya Green Crescent (YEDAM),

vinavyolenga kutoa suluhisho kwa matatizo

yanahusiana na uraibu wa madawa kwa

watu wetu, na ambayo hutoa huduma za

bure zamsaada wa kisaikolojia kwa waraibu

wamadawa na familia zao, matunda bora ya

kazi za Green Crescent yamesambazwa kote

nchini. Idadi ya vituo ambavyo vimeingia

katika huduma nchini Uturuki inaongezeka

kwa kasi. Kupitia Vituo vyetu vya Ushauri

vya Green Crescent tunawaisaidia vijana

wetu na familia zao, na tunajitahidi kuunda

hadithi za kimafanikio kuhusu matibabu ya

uraibu wa madawa na kujumuishwa kwa

watu wengine kwenye jamii.“

Green Crescent imeongoza uundaji wa mpango wa Istanbul katika jaribio la kuungana na mashirika yenye

nia sawa duniani kote katika juhudi za kuzuia uraibu, kuunda njia mpya na kuunda mkakati wa dunia. Katika

hafla ambayo iliandaliwa na Green Crescent, wawakilishi wa Mashirika 21 yasiyo ya Kiserikali (NGOs)

yanayoongoza duniani kote walitia saini tamko la pamoja na kupambana na uraibu wa dawa za kulevya.

42